MAMBO MUHIMU YA KUFANYA BAADA YA TENDO LA NDOA

 

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia siha njema na pia kwa kunipa mwangaza wa kuandika hiki ninachokusudia.
Pia niwashukuru wapenzi wasomaji wa safu hii ambao tumekuwa tukiwasiliana na kushauriana hili na lile katika tasnia hii adhimu ya mapenzi. Nawakaribisha sana!


Labda kwa wale wasiofahamu niwaambie tu kwamba dhana ya mapenzi ni dhana yenye wigo mpana sana na ndiyo maana hutasikia hata siku moja tumepumzika kuizungumzia.
 

Hata hivyo, tunachofanya siku zote ni kukumbushana kwa yale tunayoyafahamu na kushauriana kwa pale tunapohisi wengi hufanya makosa.
 

Baada ya kusema hayo sasa nigeukie mada yangu ya leo ambayo kwa kiasi kikubwa inawahusu wale walio kwenye ndoa na kikubwa nazungumzia yale ambayo wawili waliotokea kupendana kwa dhati wanatakiwa kuyafanya mara baada ya kumaliza kufanya tendo la ndoa.

Nalazimika kuandika makala haya baada ya kubaini kuwa wengi wamekuwa wakifanya makosa na kujikuta wakishamaliza kufanya tendo hilo takatifu, kila mmoja anageukie kwake kisha kuuchapa usingizi.
 

Sisemi kwamba ni lazima kuyafanya haya nitakayoyaeleza leo ila 
yakifanywa huwa na manufaa yake na mara nyingi yanaboresha uhusiano.
 

Kuoga pamoja

Mtakuwa ni watu wa ajabu kama mtamaliza kufanya tendo hilo kisha kila mmoja kulala na majasho yake. Wapowasiojali katika hili na kuona kuoga au kutooga ni uamuzi wa mtu. Elewa linapokuja suala la usafi inashauriwa mkimaliza lazima muoge.
 

Wapo wanawake ambao wakishamaliza hukimbilia kuwaandalia maji wenza wao, wakishaoga ndipo nawo huenda kuoga. Hivi unaona ugumu gani kwenda kuoga na mwenza wako? Unaijua raha ya kuoga na huyo wako wa maisha?
 

Wanaofanya hivyo wanajua raha yake na wewe ambaye hujawahi, anza leo. Mmemaliza mambo yenu, chukuaneni kimahaba, elekeeni bafuni kisha ogeshaneni kimahaba.
Baada ya hapo rudini chumbani, mkishajifuta maji pandeni kitandani mkiwa wapesi.
 

Kusifiana

Hakuna muda maalum uliotengwa kwa ajili ya wanandoa kusifiana. Hilo linaweza kufanyika wakati wowote lakini pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa ni lazima utakuwa na jambo zuri la kumuambia mwenza wako.
Msifie kwa utundu na ubunifu wake. Msifie pia kwa mapenzi matamu anayokupa na ikibidi mpe sifa ya uzuri wake kiasi cha kukufanya kila unapokuwa karibu yake ujisikie amani ya kupitiliza.
Wapo ambao hawana kabisa kasumba ya kuwasifia wala kuwashukuru wenza wao kwa mazuri wanayofanyiwa. Yaani wao wanachukulia kila kitu poa tu bila kujali kwamba kusifiana kunanogesha mambo.
 

Kuelekezana

Kwenye kale kamchezo, wapo ambao wanakosea, kuelekezana na kukosoana kwa wapenzi ni jambo la kawaida. Yawezekana mwenza wako alifanya kitu ambacho hakikukufurahisha wakati mkiendelea na burudani yenu, mnapomaliza mwambie lakini kwa lugha ya kimahaba na ya upole. Naamini kwa kufanya hivyo atakuelewa na kubadilika.
 

Zungumzieni maisha

Huu ni wakati muafaka wa kujadili changamoto na malengo katika maisha yenu. Hapa akili zinakuwa zimetulia na kila mmoja anakuwa na mawazo chanya kwa mwenza wake. Jadilini mambo yenu, wekeni mikakati ya kuliboresha penzi na maisha yenu kwa ujumla.
 

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo mnashauriwa kuyafanya pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa.
 

Yapo mnayotakiwa kuyaepuka ili kutotibua furaha iliyopatikana. Hayo nitakuja kuyaeleza katika makala zinazokuja kupitia ukurasa huu.
Soma zaidi...

VITU 10 WANAWAKE WANAVYOFIKIRIA PINDI WANAPOPISHANA NJIANI NA MWANAUME KWA MARA YA KWANZA...SOMA HAPA KIDUME KUVIFAHAMU.

 
Ngoja nikwambie wasichana hukufikiriaje wakikuona siku ya kwanza.

1.Kwanza hutazama tembea yako, kisela au kiheshima ili wajue kama una kazi au la.

2.Kama nguo zako zimefubaa unatembea juani, kama hazijanyooshwa basi hata pasi kwako huna.

3.Kama viatu vina vumbi moja kwa moja gari huna.

4.Kama pesa hutoi kwenye waleti hujazoea kuwa na pesa tena yawezekana hata laki hujawahi kushika.

5.Kama hunukii vizuri basi wanawake huwajui vizuri, na hujui romance, hata hug hujawahi kupewa.

6.Kama hutunzi nywele zako hata zake hutazigharamia.

7.Ukiongea nae muda mrefu na maswali mengi, hata kama hujamtongoza, anajua umempenda.

8. Ukimshika au kumgusa popote kwenye maongezi basi unamtaka kimwili.

9.Kama mkanda wa suruali na viatu havimachi rangi, hujawa na mwanamke kwa muda mrefu.

10. Usipomtazama machoni, yawezekana muongo au hujiamini na unamuogopa.
Soma zaidi...

ZIJUE DALILI ZA UHUSIANO WENU WA KIMAPENZI KUPOTEZA UELEKEO

 
Hatua kuu zinazoonyesha penzi limepoteza uelekeo ni hizi hapa:-
1.      MAWASILIANO KUWA DUNI
2.      USO KUONESHA KUWA HAPENDI KUONGEA
3.      HASIRA ZA MARA KWA MARA
4.      MANENO YASIYOFAA HUANZA KUZUNGUMZWA
5.      KUDAI KUTENGANA

1. MAWASILIANO KUWA DUNI

Mapenzi na sawa na jani la mti. Huendelea kuwa na mawasiliano na shina kwa kusaidiana na matawi. Ila siku ikifika jani linadondoka. Hii utokea pale jani linapochoka na maisha ya kujishikiza. Haya ndiyo sawa yalio kwetu binadamu. Mwanzo uanza kwa kasi zaidi na mwisho hufifia kwa mawasiliano. Mtu anaweza kukata mawasiliano kwa sababu zake binafsi zikiwemo hizo za hapo juu.
Kama mawasiliano yalikuwa ni mara tano kwa siku (kwa wale walio mbali, mfano masomoni.), basi mawasiliano yanaaza kushuka hadi mara mbili hadi mwisho wa siku mawasiliano kukaka kabisa. Hapa kila mmoja akiulizwa swali kwanini husema nilibanwa na kazi ndio maana sikuweza kukutafuta.
Kwa walio kwenye ndoa mawasiliano pia yanakuwa nyuma kidogo. Kama alikuwa anakusalimia kwa kukumbatiana, hapa hali hua tofauti kabisa. Muda mwingine kila mtu na kazi yake. Kila mtu shuka yake, na kukicha kila mtu kivyake.
Hii hua na athari sana pale mmoja wa wapenzi anapokuwa na mpenzi mwingine. Yule ambaye ulidhani umemchagua anakuja kuwa sumu kwako. Unapenda umwone yeye ataki. Unapenda umpe zawadi yeye ataki, unapenda kutoka naye out yeye ataki, na pale anaposema uwasiliane naye basi roho huweka pembeni. Utagundua kuwa kama analazimishwa aongee.
Ikifikia sehemu hii na kama ulimpenda kweli basi utaongeza jitihada za kutaka kuwa naye, wasio na imani hufikia mahali wanasema nitaendelea kukaa bila kuoa. Kauli hii ni udanganyifu tu. Akisahau yale yaliyomtokea, anaamua kusaka mke au mume mwingine. Unapoona hali hii imeanza jalibu kuwajilazimisha kuwa karibu yake sana. Na pale unavyoona hali ni mbaya zaidi basi mweleze rafiki yake wa karibu ambaye humwamini kwa kila jambo.
Au unaweza kumweleza mtu anayeheshimika ili asikilize kilio chako na mwisho wa siku utaona mafanikio. Hii ni kwa wachumba na hata kwa wanandoa itapotakiwa kufanya hili.
Kwa wanandoa ni muhimu wawaone pia wezee wa busara ambao wanaaminika na kukubalika na jamii. Ikishindikana basi waende katika ofisi ya kata au ustawi wa jamii kwa msaada zaidi.

 

 

2. USO HUONYESHA KUWA HAPENDI KUONGEA

Ni hali ya kawaida kuona mke au mme kuonyesha kuwa apendi kuongea na wewe. Sababu kubwa anayo moyoni na hataki kuisema. Uso mara nyingi unakuwa na asili ya mkunjo kwa wanawake. Na kwa wanaume sura inakuwa na asili na makunyanzi. Hapo ujue kuwa hali ni mbaya sana. Hapo hata ukimsesha anaona kama unajisumbua tuu. Na kama ataamua kusema ni kidogo tu na mwisho inaedelea kukaa kimwa.
Pia hata majibu yake uteyaelewa tu. Ni ya unyonge hivi, na sauti ya chini isiyo na mvuto au ushawishi kwa mwenzake. Pakifikia mahali kama hapa jalibu kumnunulia zawadi mzuri, kumkisi, kumwambia oooo mpenzi wangu….nakupenda sana…….leo umependeza namna hii….. Kweli mimi nimechagua mke mzuri au mme mzuri sana……kwani najivunia sana kukuona na kuwa na wewe muda wote.
Wakati mwingine unaweza kwenda kumsaidia kupika, kuosha vyombo na hata kumwambia mkaoge pamoja. Utaona jinsi anavyoanza kubadilika mpenzi wako. Hapa hakuna mchawi bali ni namna tabia yako ulivyomwonyesha. Hali hii haiwezi kwisha ghafla kama kimbunga bali huenda taratibu na mwisho wa siki hali inajirudia. Kwa hali ya kawaida uchukua kuanzia siku 21-22. Uendelea kumwambia maneno yenye baraka na busara bila ya kukata tama. Uwe na imanii ya hali ya juu kwani majibu utayokutana nayo si ya kawaida, lakini mwisho wa siku hali itarudi kuwa ya kawaida kabisa.

 

                                  3. HASIRA ZAMARA KWA MARA.

Hatua hii mpenzi wako huanza kuchukia kila jambo. Utende mema yeye kwake ni baya. Utajiongelesha ni kama unamuongezea hasira. Hapa ndipo watu huwa wanafikia kuchukua hatua ya kujiua wenyewe kisa mpenzi wake amamsaliti. Mfano wa majibu utayokutana nayo ni kama haya:-
  1. mbona hivi mpenzi?
  2. mimi nifanyaje?
Wewe yanakuhusu nini?
Umepata hasara gani mimi kufanya hivi?
Fanya utakavyo?
Mimi ndo kila kitu?
  1. kwa nini yamefikia hapo?
  2. we ujui?
Hizi ni baadhi ya changamoto utazokutana nazo wakati wa maojiano yako na mpenzi wako. Usimpige kisa majibu ya mkato. Kama mwanaume hali ikizidi kuwa ni kelele tu, basi kaa kimya au ondoka na kwenda kufanya shughuli zingine. Utavyorudi atashindwa anzie wapi.
Kama ni upande wa mwanamke yanamtokea haya basi fanya hivi:- kaa kimya kwa muda, atakaa kimya mpenzi wako. Kasha usisite kumwandalia mmeo chakula cha kutosha na kizuri. Hata kama hali usichoke kuandaa. Mpe maneno matamu mkiwa kitandani na kujaribu kumgusagusa sehemu mbalimbali za mwili. Hapa mwanaume ujanja unaisha hapo.
Kama hizo njia zinachukuwa muda mrefu basi anza kwa kumuomba msamaha. Hata kumpigia magoti usione aibu. Piga huku ukionyeshwa kuwa hali hile upendezwi nayo. Ni ya bahati mbaya. Hakirudi katika hali ya kawaida na siku nyingi kupita anza kushusha makombola kwa njia ya utani kuwa pale mme wangu kosa lilikuwa lako. Kama muelewa ataweza kijirekebisha ipasavyo na mwisho wa siku mukarudi kama siku ya kwanza kuanza penzi lenu.

 

4. MANENO YASIYOFAA HUANZA KUZUNGUMZWA

Hii ni hatua ya nne ambayo inahitaji uvumilivu wa hali ya juu. Mpenzi wako hutamuona mchungu kupita kiasi. Hutaona kama kuna watu wanamfundisha kuongea maneno haya. Ukweli ni kwamba ukishaona mke wako mara nyingi yeye na wenzake, hana muda wa kukaa akuandalie chakula (kwa mwanamke aliye kwenye ndoa) basi ujue kwamba rafiki zake wamemfundisha na ujue kuna jambo linaendelea ambolo mwisho wake ni kutengana.
Kwa mchumba basi utaona maneno ya ovyo ovyo ili mradi umwambie sasa mimi na wewe basi. Atafanya kila aina awezavyo utengane. Hii huweza kuwa mwanaumme ndio kisa au mke mwenyewe ndio kisa. Akishindwa hapa anaamua kuchukuwa maamuzi magumu sana ambayo hutasahau tena maishani. Kama vile kumpigia mpenzi wake mpya na kuanza kuongea naye.
Hiyo atakuwa amekuheshimu, anamkumbatia na kumkiss ili mradi uhuzunike kwa hili kasha mtenge ili awe huru. Hali hii huwa ni mbaya zaidi kama mtu umependa. Hhiki ni sawa na wanavyofanya wanaume walio wengi katika uchumba na doa. Ukimuuliza namba hii uliyosevu Juma mbona inaonyesha ni hile ya Asha atakuambia ni rafiki yangu.
Ukiendelea kumbana atakuambia ni ya mke wangu. Sasa wewe unasemaje au unataka nini? Haya utokea kwa wote wenye ndoa zao na wale walio kwenye uchumba bila kujali mme au mke au mchumba.Haya ndiyo yanayojili sehemu hii iwapo utashindwa kutatua hizo hatua tatu za mwanzo.
Namna ya kutatua sehemu hii ni kutumia zile njia elekezi ya hatua ya kwanza. Kubwa zaidi hapa ni kuomba msamaha kwa kile kinachovumilika, na kile ambacho akivumiliki ni kwenda kwa washauri nasaha kama vile maafisa ustawi wa jamii kwa manufaa ya wote. Wao watakusaidia vizuri hata kama uko peke yako na mwenza wako alikataa kwenda huko. Utamsahau na kuiona dunia ni tamu zaidi y asana na utasema mwenyewe ulichelewa wapi kipindi yanatokea haya.

 

                           5. KUDAI KUTENGANA

Kama mnavyojua, mti uota, ukua, utengeneza majani, huishi na hatimae mwisho kufa. Hapa mpenzi wako utaona ni balaa tupu. Yaani hafai hata kidogo. Kama una imani ndogo utatamani uondoke uende mbali ambako hutamwona tena. Hapa hakuna jinsi, hata mahakama huamua kutenganisha ndoa kama walioana. Hapa usipofanya kama atakavyo mpenzi wako unaweza kuishia hata gerezani au kuchukua uamuzi wa kumpiga.

Kweli inauma sana kumwona mke/mme au mchumba unaempendaanataka mutengane. Wengine huamua kujinyonga, wengine kunywa sumu, wengine wanaamia baa na kuweka makazi yao. Mmoja hakikataa hakuna jinsi, mwache aende kwa usalama.
Jinsi ya kutatua hili ni kwamba unapaswa kwenda kukubali tatizo lililotokea. Kwani kinachotokea kwa wenzako hata wewe ipo siku yatatokea. Katika maisha ya binadamu kuna kupenda na kutendwa, hivyo kutengana ni moja ya sehemu ya maisha. Jaribu kutembelea sehemu zenye mkusanyiko wa watu. Lakini usinywe pombe, na kama ulikuwa unakunya unaweza kuacha kabisa hatakwa miezi kadha na usitembelee sehemu za pombe.
Unaweza kwenda disco na sehemu nyinginezo mzuri kama vile kwenye mpira, kucheza puru, drafti, bao na hata karata. Hali yako itarudi kama zamani. Utajiona wa kawaida (hii ni kama kwa mwanaume). Ukikutana naye usimwone kama ni adui ako mkubwa, kwani yaliyotokea ni majaribu ya dunia. Na pale mkaapo kwa muda mrefu na kuona kuna umuhimu wa kurudiana basi murudiane kwa moya mmoja.
Kwa wanawake huchukua muda mrefu kama tendo lilifanywa na mwanaume. Na tatizo lenyewe kama kumfumania mme au mchumba wake wakiwa katika chumba kile kile anacholala yeye. Huwa anaona ni unyama. Kwa hili, mke huyu kurudiana naye itachukua muda mwingi kwani lile swala humrudia mara kwa mara. Na kama alimpenda sana bwana wake huamua usikuone kamwe.
Lakini hakuna jambo lisilo na mwisho. Mme unapaswa kwenda kuomba msamaha kwa yule mke wako uliyemwacha. Kukataliwa kwa mara ya kwanza ni jambo la kawaida, kwani ile icha itaendelea kumrudia. Jifanye kama usikii, fanya hivi zaidi ya mara tano hadi kumi. Mke wako au mme wako ataanza kukuonea huruma na hatimae kuwa naye pamoja.

NB: ieleweke kwamba si kila unayemfanyia tukio baya ataweza kukusamehe. Ni wachache wenye nyoyo kama hizo. Bora ubadilike na kutunza utu na uthamani wako mapema. Kwa kufanya hili maisha utayaona kama maji ya kunywa.
Soma zaidi...

JE UNAFAHAMU KWANINI WANAUME WANAONGOZA KWA KUTOKA NJE YA NDOA...?? SOMA HAPA NIKUJUZE...

 


Uvaaji wa wanawake wa namna hii huamsha hamu ya tendo la ndoa kwa mwanaume kwa kiwango kikubwa sana....
Carol Botwin ambaye ni mtaalamu anayeaminika sana kwenye masuala ya tendo la ndoa na uhusiano akiwa ameandika vitabu kadhaa kuhusu mambo hayo, kama kile cha Men Who Can’t Be Faithful, anasema, wanaume kutoka nje, siyo jambo wanalopanga, bali hujikuta tu na kujilaumu au kushangaa baadaye.
Soma zaidi...

JAMANI NITOKE NJE YA NDOA...?? NAHITAJI USHAURI WENU..

 
Nimevumilia majaribu ya ndoa yamenishinda, ninaishi na mke wangu lakini hatuna furaha yaani kama tumelazimishwa!
Hakuna kabisa furaha, tumejaribu kukaa chini na kujadili mara nyingi sana lakini huwa anadai hakuna tatizo! Najiuliza sana hivi kutoka nje ya ndoa kutanosaidia nini? Nitachinwa pesa bure na ndo matatizo yataongezeka lakini pia kiimani hairuhusiwi nami naogopa kukutwa katika dhambi na Mungu wangu!

Nimesali sana lakini kama hakuna badiliko lolote! Nimuache? Yaani kila kitu tabu tupu! Wasichana nawaogopa mno nahisi wataniongeza machungu je, nitamfute mmama wa wastani kama miaka 34 ila awe mzuri? mi nina 25. Kwakweli sijitambui niko njia panda!

Nilikuwa mwajiriwa wa kampuni fulani na nilikuwa nikilipwa laki 5 kwa mwezi sasa nina miezi 2 nkmeacha kazi sababu ya matatizo ya ndoa yangu!

Sijielewi nahisi naelekea kufa ningepata mwanamke wa umri huo na anaishi tofauti na.mji wangu na akanipenda ningeenda kukaa kwake hata kwa miezi 3.
Nahisi maisha yangu yanaharibika sasa,

Nina uchungu sana usiku huu nilikuwa safari nimerudi na zawadi zimepokelewa na kutupwa sitting rum, ninahamu nimemsogelea kitandani kanipiga pepisi jichoni nomeumia sana maana tangu tuoane sijawahi ifurahia ndoa!

Hapa najiuliza nifanyeje napanga nitoke nikalale guest lakini sina hata wakunifariji natoka naenda guest hata nikifika nikaamua kujitoa duniani inatosha.

Kuna wanawake wazuri sana, wapoleee sauti za upole akikukosea kidogo tu utasikia samahani baba yangu, nakupenda haikuwa nia yangu, jaman namimi si nipate mmoja wa hivi?
Soma zaidi...

NAITWA LUCAS NATAFUTA MCHUMBA..NA HIZI NDIZO TAARIFA ZANGU

 
Mimi naitwa LUCAS KAHIGA natokea kagera, natafuta mchumba awe na umri wa miaka 19--22 awe na Elmu ya secondary n.k. Awe mtihifu, awe na Heshima, mnyenyekevu na awe mkristo (RC) Tuwasiliane kwa namba 0787193402, 0766596264, 0713514426 na kwenye fb andika LUCAS KAHIGA.
Soma zaidi...

SIRI MUHIMU UNAZOTAKIWA KUZIJUA KUHUSU WANAWAKE!

 
Wanawake wana siri nyingi sana mioyoni mwao na kwa kawaida huwa hawawezi kuonesha hisia zao za ndani moja kwa moja. Ni watu ambao mara nyingi hupenda kuwasilisha vilivyomo ndani yao kwa ishara.
 Kwa mtindo wa maisha ya wanaume wengi wa sasa ni vigumu kusoma ishara hizo na kujua mahitaji ya mwanamke husika. Bahati mbaya ni kwamba, ukienda kinyume na mahitaji yao, utashangaa kila siku mnaingia kwenye mikwaruzano isiyo na msingi.
Wiki iliyopita nilieleza machache, leo tunaingia katika sehemu ya mwisho. Hebu fuatilia kwa makini ujue mwanamke anapenda vitu gani hasa ili uweze kuishi naye kwa amani.
KUSIKILIZWA
Ukitaka kumpatia mwanamke, msikilize. Kumbuka wanawake wengi wana hulka ya kuongea sana! Ndivyo walivyo.
Wakati fulani, mwanamke anapenda kuzungumza mambo fulani na mwanaume wake.

Pengine anapenda kumshauri au kujadiliana naye jambo fulani; huenda ana mawazo mazuri lakini mtindo wao wa kuongea sana unaweza kukatisha tamaa. Usifanye hivyo. Mpe nafasi.
Msikilize kwa makini, mwishowe unaweza kupata manufaa makubwa kutokana na maneno yake. Amini usiamini, hata katika mambo yanayohusu mafanikio, ukimshirikisha mkeo, huwa na mawazo mazuri yanayochochea kuifukuzia ndoto yako.
Ukiachana na hilo, mwanamke anaweza kukuambia, hapendi mavazi yako – hapendi nguo fulani unayovaa, labda kwa hoja kuwa haikupendezi! Usimdharau. Sikiliza hisia zake.
Kumbuka upo kwa ajili yake, anaweza kujiuliza, kama anakuambia mavazi hayo si mazuri kulingana na umbo lako na ung’ang’ania, unamvalia nani huko nje? Msomaji mmoja aliwahi kuniambia: “Yaani kaka Shaluwa, mume wangu ananishangaza sana.
“Anapenda kuvaa suruali za vitambaa, pana na mashati makubwa kama Mzaire. Nimeshamwambia mara nyingi kuwa sipendi na hapendezi, lakini bado analazimisha kuvaa. Ananinyima raha sana, maana hata nikiongozana naye, nakuwa kama nipo na mtu mzima!”
Unaweza kuona namna gani wanawake wanavyokereka na mambo madogo tu lakini wakiyapa uzito 
wa hali ya juu.
MSIMAMO
Wanawake wanapenda mwanaume mwenye kujiamini na kusimamia msimamo wake. Unaweza kushangaa lakini wakati mwingine mwanamke anaweza hata kukuweka kwenye mtego; mnakubaliana jambo lakini baadaye anajifanya kukupinga ili kuona msimamo wako.
Wanaamini katika mwanaume anayejielewa na asiyeyumba wala kuyumbishwa. Kwamba, mwanaume wa aina hiyo ni rahisi kufikia ndoto za familia – yeye kama kiongozi wa nyumba.
ZAWADI
Si lazima ununue gari jipya na kumpelekea kama zawadi. Kumchagulia wimbo mzuri redioni, kadi yenye mashairi mazuri ya kimapenzi, bangili, vipodozi na vitu vingine vidogovidogo huwafurahisha sana wanawake.
MTOKO
Hata kama ni mara moja baada ya miezi miwili, ukitoka na mwenzako na kwenda naye kupata chakula cha jioni mgahawani huongeza mapenzi. Kwa mwanamke ni jambo kubwa lenye thamani sana.
Soma zaidi...

HAYA NDIO MADHAIFU MATANO (5) YANAYODIDIMIZA MAHUSIANO NA NDOA

 
Makalahii ni tafakari huru kuhusu mambo ya msingi katika mahusiano. Hapa utapata tafakari ya maana ya maneno naimani ambazo zinatutatiza wengi wetu. 1. Mchanganyiko mkubwa kuhusu maana yamahusiano, mapenzi na ndoa: Labdakipengele hiki tuanze kwa kueleza kuwa kunaweza kuwepo ndoa, lakini yasiwepomahusiano... wala mapenzi. Inaweza kuonekana kama inachanganya kidogo, lakini ndioukweli wenyewe. Ndoa ni namna tuu ambayowawili walio kwenye
mahusiano wanaamua kuwataarifu rasmi watu wengine kuwa waowapo rasmi katika mahusiano. Ndoa ni kiapo mbele ya watu wengine , na ni namnaya kutaka kumuhakikishia mwenza wako kuwa endapo kiapo hicho kitatokeakuvunjika, basi unakubali rasmi kuwajibika kwa mujibu wa taratibu zilizopo zandoa husika, ikiwemo kukubali kuitwa kwenye mabaraza ya usuluhishi, kugawanamali, n.k. Na kwa upande wa kiroho, inabeba maana zaidi kuwa unaweka kiapo kwaMungu wako kuwa utalinda mahusiano yako na huyo unayemchagua. Hivyobasi, ndoa haijengi mahusiano wala mapenzi.
Kiuhalisi inabidi kwanza yawepomahusiano na mapenzi kisha ndio kiapo kifanyike, kwani kinyume
cha hivyo nikuwa unakula kiapo 'feki'. Ndiomaana basi, ni muhimu kwa wapenzi kutambua kweli kama wanahitajiana, kuwakwenye mahusiano na kutafakari kwa uhuru kama kweli wanataka kuweka kiapo rasmicha kuwa pamoja. Kutumiandoa kama kinga ya kuhakikisha mahusiano yako yanadumu ni maamuzi magumu ambayopengine yanaweza yasilete faida hapo baadae.

2.Mahusiano na ndoa nyingi huyumbishwa naMatarajio yasiyo halisi Kablahata ya kuingia katika mahusiano na hatimaye ndoa wengi wetu huwa na matarajiobinafsi ya kimaisha. Matarajio haya yanajumuisha vile tunavyotaka sie wenyewekuwa hapo baadae, pamoja na matarajio ya vile tunavyotaka wenza wetu wawe. Hatahivyo katika hali

halisi tunajikuta sisi wenyewe hatuwezi kujibadilisha aukujiweka kwa usahihi vile tunavyotamani kuwa (kwa sababu kwa kila tunachojaribukufanya kuwa bora, tunajikuta bado tuna madhaifu mawili matatu). Pamoja naukweli huu, tunajikuta tupo na matarajio ya kuwafanya wenza wetu wawe watu waaina fulani. Kwakuwa kiasili binadamu ni kiumbe huru, tunajikuta wenza
wetu naowakiwa 'busy' kutimiza ndoto za vile wanavyotamani kuwa iwe kimavazi, aina yamarafiki,
utafutaji wa kazi , kujiendeleza kimasomo, aina ya mali za kununua,hata kufikiria tofauti aina ya maisha wanayotaka muishi. Matokeoyake ukinzani huu wa matarajio ni mkanganyiko wa mgongano wa mawazo kati yawawili nyie, na mwanzo wa vita ya chini kwa chini ya nguvu ya maamuzi katikamahusiano yenu.

3. Kuweza kumbadili tabia mwenza wako Mojawapoya jambo ambalo hufanywa na wengi walio katika mahusiano ni kuwa na 'tamaa' yakutaka kumbadili tabia fulani mwenza wake. Hata hivyo 'tamaa' hii ni sehemu yayale tunayoyaita matarajio yasiyo halisi, kwani tabia ya mtu hujengwa na mambomengi sana, ikijumuisha aina ya makuzi, aina ya mfumo wa imani mtu anaouamini,aina ya marafiki alio nao, uwezo wake wa kujiamini katika kubadili tabia kwaniwengine wameshakata tamaa kuwa hawawezi kukata tamaa, na zaidi sana, mabadilikoya tabia huhitaji mfumo endelevu na wenye kusoma vema asili ya tabia ili kuwezakuirekebisha. Hatahivyo wengi wetu kwenye mahusiano, hutegemea 'mapenzi'au vitisho tuu kama
vile'nitakuacha mie ', kama sababu yakumfanya mtu abadilike kitabia.Udhaifu wetu katika kutambua asili
ya tabia yamtu husika na mbinu za kisayansi za kubadili tabia hufanya zoezi lakubadilishana tabia kuwa gumu na pengine lisilowezakana.

4. Kuvumilia ndio kuonyesha upendo na ndiokudumisha mahusiano Hiini aina nyingine ya matarajio ambayo sio halisi kwani kiukweli kila mtu analojukumu la kufanya bidii kuwa mtu mwema, hivyo hauhitaji kubeba 'uzembe' wamwingine kwa kisingizio tuu cha kuwa unaonyesha upendo hususani pale ambapo nikwa
uzembe tuu au kutokujali kwake mwenza husika amefanya jambo fulani. Kwajinsi kasumba hii ilivyo enea sio ajabu kukuta mtu akifanya mambo mabaya kwamwenza wake kwa makusudi ili tuu eti apime kama kweli mwenza wake ni mvumilivu. Kumbukahapa hatumaanishi kuwa kusamehe ni kosa. Hapana, kusameheana ni muhimu, lakinisio kwamba ni muhimu tuu katika mapenzi. Kusameheana ni jambo la asili, natunapaswa
kusameheana kwa mambo mengi nje hata ya mahusiano.
Tunachosemani kuwa kuna kasumba ya baadhi yetukuona kuwa wanayo 'haki' ya msingi ya kukosea eti tuu kwakuwa tuu mwenza wakeanalazimika kusamehe ili kuonyesha kweli anao upendo wa dhati. Amini usiamini, kasumba hii ya kutarajia ainaya pekee ya kusamehewa na kuvumiliwa kwa kisingizio
tuu cha kuwa upo kwenyemapenzi namwenza wako, hurudisha nyuma maendeleo ya mahusiano yenu kwanimwenzi wako nae ni binadamu na kumbuka anayo matarajio mengine ya maisha,isitoshe na yeye anahitaji upendo na
kujaliwa na wewe, hivyo kutarajia kwakokusamehewa na kuvumiliwa kuna mnyima haki mwenza wako. Hatimaye kutegema kwakokusamehewa kila wakati, kunamfanya mwenza wako atilie mashaka upendo wakokwake.

5. Uaminifu = Upendo= Kudumu kwa mahusiano Pamojana ukweli kuwa mwenza wako anatarajia utakuwa muanifu kwake, elewa kuwa kuwamwaminifu pekee katika mahusiano yako sio tiketi ya kudumu kwa mahusiano yenukwakuwa watu wanaingia kwenye mahusiano sio tuu kwa kuwa wanataka kuwa na mtummoja muaminifu bali wana mahitaji mengine wanayohitaji. Zungumzana mwenza wako, fanya utafiti wako binafsi kuhusu mpenzi wako ujue mambomengine anayohitaji toka kwako. Pia msikilize anapokutaka urekebishe mambokadhaa au ufanye mambo fulani. Inapendeza pale unapomfanyia mtu
mamboyanayompendezesha kwa kuwa hivyo ndivyo anavyotaka, sio kwakuwa tuu weweunadhani kufanya hivyo kutampendezesha mhusika.
Soma zaidi...

NAITWA CANNRY HOJANE NATAFUTA MCHUMBA ..HIZI NDIZO TAARIFA ZANGU

 
natafuta mchumba manake nimekaa miaka mingi sasa sina mchumba kwa sasa nmemaliza chuo miaka mitatu na digri ya sheria mimi nakaa maeneo ya kurasini dar es salaam na 0719931626 ni namba yang ya simu ,napenda mwanamke yeyote mwenye umri sawa na mm wa miaka 21 au 20 wa rang yoyote,kabila lolote,mtiif,mwny heshm kwa mdogo au mkubwa mwanamke yeyote aliyevutiwa na habar zang anaestahili asisite kunipigia hiyo namba na email ni bynfryn@yahoo.com

Soma zaidi...

NAITWA KISSABA EMANUEL NATAFUTA MCHUMBA ATAKAYE KUWA MKE WANGU..NA HIZI NDIZO TAARIFA ZANGU

 
 
Natafuta mchumba ambaye atakuwa mke na mama wa watoto wetu. Umri miaka 30-36. Mkristo, anasali na kumjua Yesu. Elimu ya Secondary na kuendelea......awe mfanyakazi....ningependelea zaidi Mwalimu. Anayependa kujiendeleza. Mawasiliano ni ekissaba@gmail.com ama 0657 353565 (sms only) Usi-beep
Soma zaidi...